Home BIASHARA NMB yashiriki Wiki ya Ubunifu Tanzania 2023

NMB yashiriki Wiki ya Ubunifu Tanzania 2023

Google search engine
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kati, Nsolo Mlozi, akimueleza jambo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, alipotembelea Banda la NMB kuhusu namna wanavyofanyakazi Kidigitali katika Viwanja vya Jamhuri jijini Dodoma.

NA MWANDISHI WETU

-DODOMA

KATIKA kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kupitia Wizara ya Sayansi, Elimu na Teknolojia,Benki ya NMB imedhamini na kushiriki Wiki ya Ubunifu Tanzania 2023 yenye kauli mbiu ya ‘Ubunifu kwa Uchumi Shindani’ inayofanyika viwanja vya Jamhuri jijini Dodoma.

Ushiriki huo una lengo la kuwawezesha wabunifu kujionea na kujifunza bunifu za kiteknolojia za masuluhisho ya kifedha, na kuweza kujaribu masuluhisho yao kupitia mfumo wa ‘NMB Sandbox environment’ ambayo inatoa fursa kwa wabunifu wa masuala ya kifedha kuweza kufanya majaribio ya bunifu zao na kisha kuwasaidia wabunifu hao kuingia sokoni.

Benki hiyo imetenga kiasi cha Bilioni moja kwa ajili ya kuwasaidia wabunifu wanaochipukia kuweza kuziweka bunifu zao katika utekelezaji ili waweze kunufaika, lakini kiasi hicho sio mkopo bali ni fedha iliyotengwa kwa dhumuni ya kusaidia wabunifu hao na hawatawajibika kuirejesha.

Benki hiyo ipo kwenye viwanja vya Jamhuri Dodoma wiki nzima. Tembelea banda lao kujua zaidi kuhusu suluhishi za kidijitali.

Google search engine

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here