Home KITAIFA WANANCHI WAKARIBISHWA KUTEMBELEA BANDA LA WIZARA YA FEDHA SABASABA

WANANCHI WAKARIBISHWA KUTEMBELEA BANDA LA WIZARA YA FEDHA SABASABA

Google search engine
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Jenifa Omolo(wa kwanza kulia) akizungumza jambo na Afisa Mwandamizi Usimamizi Masoko wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Antony Kashube alipotembelea banda la Wizara ya Fedha katika katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, yanayoendelea katika viwanja vya sabasaba, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Jenifa Omolo (kushoto) akipitia vipeperushi vya Taasisi ya Usuluhishi wa Malalamiko ya Kodi alipotembelea banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, yanayoendelea katika viwanja vya sabasaba, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam, kulia ni baadhi ya maafisa wa Wizara hiyo
Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 na Spika wa Bunge Mstaafu, Anne Makinda akisaini vitabu vya wageni alipotembelea banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, yanayoendelea katika viwanja vya sabasaba, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Miriam Mahuwi na kushoto ni Issa Magabiro kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS).

Na Farida Ramadhani, WF

– Dar es Salaam

Wananchi wamekaribishwa kutembelea banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, yanayoendelea katika viwanja vya sabasaba, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam, ili kupata elimu ya huduma mbalimbali zinazotolewa na Wizara hiyo pamoja na baadhi ya taasisi zilizo chini yake.

Wito huo umetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Jenifa Omolo alipotembela banda hilo na kuzungumza na waoneshaji kutoka Wizara na Taasisi zake.

Alisema katika banda hilo wananchi watapata elimu kuhusu Bajeti Kuu ya Serikali na uandaaji wake, sera mbalimbali za usimamizi wa kodi, usimamizi wa mali za Serikali, mifumo ya malipo na mishahara.

“Kuna taasisi za elimu ambazo zinawawezesha wahitimu kujitegemea baada ya kumaliza masomo yao lakini pia kuna taasisi za fedha na zinazojihusisha na uwekezaji”, alibainisha Omolo.

Alisema banda hilo linatoa elimu ambayo itamuwezesha mwananchi kujua namna Serikali inavyopanga mipango mbalimbali ya maendeleo, inavyosimamia miradi ya maendeleo pamoja na ujenzi wa miundombinu.

Afisa Mtendaji wa Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA), Prof. Geraldine Rasheli akisaini kitabu cha wageni katika banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, yanayoendelea katika viwanja vya sabasaba, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Muhtasi wa Wizara ya Fedha, Masia Msuya.

Omolo alibainisha kuwa wananchi watapata elimu kuhusu mifumo mbalimbali iliyoanzishwa na Serikali kwa ajili ya kusimamia fedha na kuongeza ufanisi katika kutekeleza majukumu yake.

Kwa upande wa baadhi ya wananchi waliotembelea banda hilo waliipongeza Serikali kwa kuweka maonesho hayo ambayo yamewaezesha kujua mambo mbalimbali yanaotekelezwa na Serikali hususani masuala ya usimamizi wa fedha na kukuza uchumi.

Wameshauri elimu hiyo iwe endelevu hata baada ya kumaliza maonesho hayo kwa kuwa wananchi wengi bado hawanauelewa wa mambo mengi yanayotekelezwa na Serikali.

Google search engine

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here