Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Fatuma Mwassa (wa pili kutoka kushoto) akipokea mfano wa hundi ya shilingi milioni 50 kutoka kwa Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kati, Nsolo Mlozi ( pili kutoka kulia) kama ufadhili wa Benki hiyo katika sherehe za Mei Mosi ambazo kitaifa zitafanyika Mkoani Morogoro. Kushoto ni Meneja wa benki ya NMB tawi la Wami, Horold Lambileki na kulia ni Afisa Rasilimali watu wa Benki ya NMB kanda ya Kati, Bryson Tarimo.