Home KITAIFA Serikali kuendelea kuboresha mazingira ya biashara nchini

Serikali kuendelea kuboresha mazingira ya biashara nchini

Google search engine
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Lawrence Mafuru akibadilishana mawasiliano na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC), Takashi Araki baada ya kumaliza kwa kikao kati ya Serikali na Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) kilichofanyika jijini Dodoma.

Na Joseph Mahumi WFM, Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru,  amewahakikishia  wafanyabiashara na makampuni binafsi kwamba Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya biashara nchini ili kuwawezesha kuendelea kuwekeza na kukuza uchumi wa nchi.

Bw. Lawrence Mafuru ametoa ahadi hiyo alipokutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC), Takashi Araki.

Mafuru alisema Sekta Binafsi ina imani na Serikali hali ambayo inawawezesha wawekezaji kuwa na uhakika na mipango yao.

“Kampuni ya Sigara nchini wamefurahishwa na Sera za usimamizi wa uchumi ambazo zimeendelea kuboreka na kuwawezesha kufanyabiashara yenye tija”, alisema Mafuru.

Alisema pia kuwa Kampuni hiyo umeelezea kufurahishwa kwao na mazingira ya siasa yalivyo, ambayo yanaruhusu amani na utulivu huku wakiiomba Serikali kuangalia vikwazo mbalimbali vinavyokwamisha ufanyajibiashara nchini kwa ufanisi zaidi.

Alisema wameshauri Serikali iangalie suala la kodi kwa kuwa na kodi ambazo zinatabirika na zisizobadilikabadilika kila wakati pamoja na kuangalia mazingira mengine ya ufanyaji biashara.

Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC), Takashi Araki (kulia), Mkurugenzi wa Mahusiano wa Kampuni hiyo, Patricia Mhando (katikati) na Meneja Mahusiano wa Kampuni hiyo, Bw. Derick Stanley wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Lawrence Mafuru (hayupo pichani) katika kikao kati ya Serikali na Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) kilichofanyika jijini Dodoma.

Nae Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC), Takashi Araki alisema kampuni hiyo itaendelea kushirikiana na Serikali katika kukuza uchumi wa nchini huku akisisitiza kuhusu kujenga uaminifu kati ya Serikali, Sekta Binafsi na wananchi.

Alisema ni jambo la msingi kuwa na uchumi unaokua na kuhusisha maendeleo ya watu, hivyo anatamani Tanzania iwe na uchumi thabiti.

Naibu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC), Takashi Araki wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara ya Fedha na Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC), baada ya kumaliza kwa kikao kati ya Serikali na Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) kilichofanyika jijini Dodoma
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru akiongoza kikao kati ya Serikali na Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) kilichofanyika jijini Dodoma.
Google search engine

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here