Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amekutana na Waziri wa Uhamiaji , Sheria na Haki za Walaji Jimbo la Thuringia Ujerumani Mhe. Doreen Denstadt mwenye asili ya Kitanzania, katika mazungumzo yao wamegusia kuanzisha ushirikiano baina ya Jimbo la Thuringra na Tanzania pia baina ya Mji wa Weimer na Zanzibar.